Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (ABNA), Ayatullah Nouri Hamedani amesisitiza umuhimu wa kuzingatiwa kwa masharti na miongozo iliyowekwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu mazungumzo na masuala ya kitaifa.
Akizungumza katika mkutano wake na Mkuu wa Ofisi ya Rais wa Iran, Ayatullah Nouri Hamedani amesema kuwa ni lazima kanuni za “Heshima (Izzah), Hekima (Hikmah) na Maslahi (Maslahah)” ambazo zimekuwa zikisisitizwa na Kiongozi wa Mapinduzi, zipewe kipaumbele katika maamuzi na sera za nchi.
Ameongeza kuwa mipaka na miongozo iliyochorwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu inapaswa kuheshimiwa na kutekelezwa kwa umakini mkubwa, huku akibainisha kuwa sera kuu za mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu huamuliwa na Kiongozi wa Mapinduzi na jukumu la viongozi na maafisa wa serikali ni kuzitekeleza kwa ufanisi.
Ayatullah Nouri Hamedani pia alisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano katika kulinda maslahi ya taifa na kuimarisha nafasi ya Iran katika nyanja za kikanda na kimataifa.
Your Comment